Skip to main content

AZIZ KI AKATA MZIZI WA FITINA

Sports and Games

"Wanaomuhitaji Aziz Ki wapo vizuri kifedha hiyo ni kweli sina haja ya kuleta propaganda mimi nimenyooka kama rula, mimi ningekuwa mtu wa propaganda ningewaambia Aziz kasaini ila ukweli bado hatunae, hakuna siasa hapa tusipeane moyo wakati uhalisia tunaukimbia."- Ally Kamwe, Afisa habari wa klabu ya Yanga SC.

Taarifa kutoka ndani ya Yanga SC inasema Vilabu vya Afrika kusini na Uarabuni ndivyo vilivyotuma ofa kubwa kumuhitaji Aziz Ki, klabu ya Yanga bado iko mezani na Mchezaji huyo wakifikia makubaliano ya kumbakiza watasema, wakishindwa pia watasema.

Pia inatajwa ofa iliyotumwa, Pesa ya usajili "Signing fee" na mshahara kwa miaka mitatu (3) na klabu moja kubwa kumsajili Aziz Ki ambapo thamani yake inakaribia kufikia Shilingi Bilioni mbili za kitanzania.

Toa maoni yako

By Maximilian Damian reporter



Follow us on

YouTube

Facebook


Comments

Popular posts from this blog

TETESI: Klabu ya Yanga SC imepanga kuachana na Nyota wake 6 ambao ni Mghana Agustine Okrah, kiungo Mahlatse Skudu Makudubela

YANGA SC NEWS UPDATE #TETESI: Klabu ya Yanga SC imepanga kuachana na Nyota wake 6 ambao ni Mghana Agustine Okrah, kiungo Mahlatse Skudu Makudubela kutoka Afrika Kusini, Mkongo Joyce Lomalisa, Zawadi Mauya, Metacha Mnata na Joseph Guede kutoka nchini Ivory Coast. Taarifa za ndani zinasema tayari wa Uongozi wa Yanga SC wamemaliza kuwaongezea mikataba nyota wote watakaosalia kikosini hapo kwa msimu 2024-25 lakini majina va wachezaji hao sio sehemu ya wachezaji waliongezewa mikataba kuelekea msimu ujao wa Mashindano ndani ya Yanga SC. Yupi alistahili kubaki ndani ya Yanga msimu ujao hapo??

Kiungo wa Yanga Sc, Stephanie Aziz Ki amekata mzizi wa fitina juu ya mustakabali wake kufuatia taharuki

Sports and Games Kiungo wa Yanga Sc, Stephanie Aziz Ki amekata mzizi wa fitina juu ya mustakabali wake kufuatia taharuki iliyozuka miongoni mwa wapenzi wa soka baada ya posti yake aliyochapisha kwenye mitandao ya kijamii kuzua sintofahamu. Awali kiungo huyo raia wa Burkina Faso alichapisha taarifa ya kuushukuru uongozi wa klabu hiyo, mashabiki pamoja za wachezaji wenzie kwa mafanikio waliyoyapata katika msimu uliomalizika hali iliyopelekea wengi kudhani anaaga Yanga. Hata hivyo Aziz Ki amejibu 'comment' ya mdau iliyosema “Ashiiii Azizi sasa kwenye post yako usianze na maneno 'thanks' unatufanye tuhofie kuwa unataka kuondoka” Akijibu 'comment' hiyo Ki ameandika “Nawashukuru kwa sababu ni jambo dogo sana ninaloweza kufanya kuwashukuru nyinyi ambao mnanisaidia kila siku, SIO KWAHERI NIKO HAPA MSIJALI” Posti iliyozua sintofahamu ilisomeka "Kila kitu kiliwezekana Shukrani kwenu wachezaji wenzangu, wafanyakazi, kamati ya rais na hasa nyinyi mashabiki, wapendwa wa...

BREAKING NEWS YANGA SC YAONDOLEWA ADHABU NA FIFA

Sports and Games Taarifa kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) @taifastars_ @caf_online @yangasc By Maximilian Damian reporter Follow us on Facebook