Skip to main content

DROO YA KUWANIA KOMBE LA AFCON YAWE KWA WAZI

YANGA SC NEWS UPDATE


DROO ya kuwania kufuzu kombe la Mataifa Afrika 2025, AFCON 2025 imefanyika leo Julai 4, 2024 Jijini Johannesburg, Afrika Kusini ambapo timu za Mataifa 48 yamebaini wapinzani wao kwenye hatua ya makundi kwa toleo la 35 la michuano hiyo inayofanyika kila baada ya miaka miwili.

Timu ya taifa ya Tanzania imepangwa kwenye Kundi H sambamba na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Guinea na Ethiopia huku Mabingwa watetezi, Ivory Coast wakipangwa Kundi G sambamba na Zambia, Sierra Leone na Chad.

Wenyeji wa michuano hiyo, Morocco wamepangwa Kundi B sambamba na Gabon, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Lesotho.

MAKUNDI 

Group A: Tunisia, Madagascar, Comoros, Gambia
Group B: Morocco, Gabon,Central Africa Republic, Lesotho 
Group C: Egypt, Cape Verde, Mauritania, Botswana
Group D: Nigeria, Benin Libya, Rwanda 
Group E: Algeria, Equatorial Guinea, Togo, Liberia
Group F: Ghana, Angola, Sudan, Niger
Group G: Cote d'Ivoire, Zambia, Sierra Leone, Chad
Group H: DR Congo, Guinea, Tanzania, Ethiopia
Group I: Mali, Mozambique, Guinea Bissau, Eswatini
Group J: Cameroon, Namibia, Kenya, Zimbabwe
Group K: South Africa, Uganda, Congo, South Sudan
Group L: Senegal, Burkina Faso, Malawi, Burundi.


Comments

Popular posts from this blog

Klabu ya Yanga SC imefanya uzinduzi wa jezi mpya watakazotumia kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika 2024/25 Unazipa Marks ngapi kati ya 10____?

YANGA SC NEWS UPDATE Klabu ya Yanga SC imefanya uzinduzi wa jezi mpya watakazotumia kwenye michuano ya Klabu Bingwa Afrika 2024/25 Unazipa Marks ngapi kati ya 10____? Young Africans SC  𝐂𝐀𝐅𝐂𝐋 πŸπŸŽπŸπŸ’/πŸπŸ“ - π“π‡πˆπ‘πƒ πŠπˆπ“πŸ”° #TimuYaWananchi  #DaimaMbeleNyumaMwiko

TUZO ZA TFF KUTOLEWA LEO KATIKA UKUMBI WA SUPER DOME MASAKI

YANGA SC NEWS UPDATE ... 🚨 π—¨π—£π——π—”π—§π—˜π—¦ ℹ️ Tuzo za (TFF) zitafanyika   1 Aug 2024 katika ukumbi wa Super Dome Masaki.  Zaidi ya watu 550 watahudhulia.  ℹ️ Bodi ya ligi kuu Tanzania bara imesema kuwa, wamechelewa kutoa ratiba ya ligi kuu kwa sababu ya confirmation ya viwanja.  Bodi hiyo imeeleza kuwa, 24 | 25 wamepanga kutumia viwanja vichache ambayo ni bora ili kulinda hadhi ya ligi kuu Tanzania bara.

TAARIFA NJEMA KWA YANGA SC

YANGA SC NEWS UPDATE Hii inaweza kuwa habari njema kwa Yanga baada ya taarifa kutoka Algeria kubainisha kwamba mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika Kundi A dhidi ya MC Alger utachezwa palepale ulipopangwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na si vinginevyo. . Awali MC Alger kupitia rais wa klabu hiyo, Mohamed Hakim walipeleka barua CAF kuomba kubadilisha uwanja wa mechi kutoka 5 July 1962 na wakitaka kuutumia Ali la Pointe, lakini ombi lao limekataliwa.  . Mechi hiyo imepangwa kuchezwa Jumamosi, wiki hii. Uwanja wa 5 July 1962 uliopo katika Mji wa Algiers ni karibu zaidi na Uwanja wa Ndege wa Houari Boumediene ambao Yanga itatua leo mchana ikitokea Dar es Salaam, hivyo haitawapa wakati mgumu wa kuanzisha safari nyingine kwenda Douera unapopatikana Uwanja wa Ali la Pointe.  . Hata hivyo, MC Alger waliangalia mbali zaidi kwani Uwanja wa Ali la Pointe ndiyo wanautumia zaidi kwa mechi za nyumbani za ligi, hivyo wameuzoea zaidi kulinganisha na 5 July 1962. Kitendo cha CAF kutokuba...